Monday, March 31, 2014

JEZI MPYA ZA ENGLAND ZITAKAZOTUMIKA KOMBE LA DUNIA




Uingereza wametoa jezi mpya za nyumbani na ugenini ambazo watatumia kwenye kombe la dunia mnamo mwezi 6 mwaka huu huko Brazil. Jezi hizo zimetengenezwa na kampuni ya Nike, ambapo Uingereza watatumia jezi zenye rangi nyeupe kama za nyumbani na nyekundu kama za ugenini. Jezi hizo zitaanza kuuzwa tarehe 3 mwezi wa nne.
Kwa upande mwingine, wadadisi hasa wapenzi na mashabiki wa Uingereza wanajiuliza hawa wachezaji Ross Barkley, Raheem Sterling na Alex Oxlade Chamberlain, Gerald, Hart, Wilshere na Sturridge ambao wametumika kwenye hizi picha za kutangaza jezi, Je ndio tayari wamepata tiketi ya kwenda kule Brazil? Utata unakuja zaidi kwa mcheaji wa Everton Barkley ambaye kabla alionekana ni 50/50 kuitwa kwenye kikosi au kuachwa. Tusubiri tuone.



No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...