Simba
 ilifanya vitendo hivyo katika mechi yake dhidi ya Mbeya City ambapo 
imepigwa faini ya sh. 500,000. Pia imepigwa faini nyingine ya sh. 
500,000 kwa makocha wake Loga, Selemani Matola na Idd Pazi kuingia 
uwanjani na kumzonga mwamuzi kwenye mechi hiyo.
Naye
 mshambuliaji wa Simba, Amisi Tambwe amepigwa faini ya sh. 500,000 kwa 
kushangilia bao alilofunga kwenye mechi hiyo kwa kuonesha ishara ya 
matusi kwa kidole.
Mbeya
 City imepigwa faini ya sh. 300,000 kwa washabiki wake kuingia uwanjani 
kwenye mechi dhidi ya Kagera Sugar iliyochezwa mjini Bukoba. Klabu za 
Yanga na Coastal Union zimepigwa faini ya sh. 500,000 kila moja kwa 
washabiki wao kurusha chupa za maji uwanjani wakati timu hizo 
zilipopambana jijini Tanga.
Kiungo
 wa Mtibwa Sugar, Shabani Nditi amepigwa faini ya sh. 500,000 kwa 
kumpiga mchezaji wa Simba, wakati Salvatory Ntebe pia wa Mtibwa Sugar 
amepigwa faini ya sh. 500,000 kwa kumtukana refa kwenye mechi dhidi ya 
Mbeya City.
Pia
 mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Musa Mgosi amepigwa faini ya sh. 500,000 
kwa kosa la kupiga uwanjani kwenye mechi dhidi ya Ashanti United ambapo 
vilevile atakosa mechi tatu za ligi. Coastal Union imepigwa faini ya sh.
 500,000 kwa washabiki wake kumrushia chupa za maji kipa wa Mbeya City.
Nayo
 JKT Ruvu imepigwa faini ya sh. 300,000 kwa kuchelewa kufika uwanjani 
kwenye mechi dhidi ya Simba iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Vilevile
 wamiliki wa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wameandikiwa barua ya 
kufanya marekebisho ya vyumba vya wachezaji, kwa vile havina hewa ya 
kutosha.
Kwa
 upande wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) klabu zilizopigwa faini kutokana 
na makosa mbalimbali ni Friends Rangers (sh. 200,000), Lipuli (sh. 
200,000), Majimaji (sh. 400,000), Polisi Morogoro (sh. 400,000) na 
Transit Camp (sh. 200,000).
Kocha
 Msaidizi wa Polisi Morogoro, John Tamba atapelekwa kwenye Kamati ya 
Maadili kutokana na vitendo visivyo vya kimaadili katika mechi dhidi ya 
Burkina Faso.
Kiongozi
 wa Lipuli, Hamis Kiemba na wachezaji Boniface Sawaka, George Enock na 
Green Paul watapelekwa katika Kamati ya Nidhamu kutokana na utovu wa 
nidhamu waliofanya kwenye mechi dhidi ya Kimondo.
Naye
 mchezaji Sangalau Nyamoka wa JKT Kanembwa aliyelalamikiwa uhalali wake 
na Polisi Tabora suala lake linapelekwa Kamati ya Nidhamu.
No comments:
Post a Comment