TAMKO LA KKKT KUHUSU KATIBA MPYA
 
Msaidizi
 wa Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kikristo Tanzania (KKKT), Dayosisi 
ya Dodoma Mchungaji Samweli Mshana, amewataka wajumbe walio katika 
mchakato wa Katiba kuhakikisha wanawapatia watanzania Katiba itakayotoa 
haki zote bila upendeleo. 
Aidha, alisema kanisa hilo halitarajii Katiba hiyo kumilikiwa na vyama vya siasa na viongozi wao au kuwa ya kiitikadi. 
Mchungaji Mshana alisema hayo akizungumza katika tamasha la akinamama KKKT Jimbo la Makao Makuu, Dodoma. 
Mchungaji huyo alisema hatarajii kuona wajumbe hao wakijadili Katiba kwa kupendelea upande wowote ule wa jamii. 
Naye 
Mwenyekiti wa Wanawake Jimbo la Makao Makuu KKKT Dodoma, Salome Kingu 
alisema wanawake wa jimbo hilo tangu lianze Bunge hilo la Katiba 
wamekuwa wakimlilia Mungu ili Katiba iweze kuwa ya Watanzania wote na 
itakayojali haki. 
Katika
 tamasha hilo mafundisho mbalimbali yatafundishwa ikiwemo somo la 
Maadili ya Mwanamke katika kanisa na Ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia 
kwa wakati huu tulionao na somo la Maadili ya Wanawake, Sheria na 
Mirathi.
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment