MAMLAKA
 ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema kuwa asilimia 79 ya simu za 
kiganjani zilizofanyiwa utafiti kwa kipindi cha desemba hadi February 
mwaka huu ziko salama na sio za bandia ,huku asilimia 18 zikionekana 
zikiwa za bandia hivyo kuwataka wananchi kutambua kuwa simu feki 
zilizoko sokoni ni chache tofauti na kipindi cha nyuma. 
Pia
 imebainika kuwa asilimia kubwa ya nyumba zinazoungua na umeme ni 
kutokana na simu bandia ambazo betri zake au vifaa vyake hushindwa 
kuhimili  mionzi pindi zinapokuwa zinachajiwa hivyo kusababisha mlipuko 
wa moto na hivyo kuleta madhara . 
Hayo
 yalisemwa na meneja uhusiano wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania 
Innocent Mungi alipokuwa akizungumza katika semina ya mfumo wa rajisi 
ya  namba za utambulisho wa simu za kiganjani iliyowashirikisha wadau na
 wafanyabiashara wa jijini hapa. 
Alisema
 kuwa kutokana na elimu ambayo wameitoa kwa wafanyabiashara wa simu  
hizo ya kuhakiki kwanza kabla ya kuwauzia wananchi imepunguza uingizaji 
wa simu feki na kwamba wamebaini kuwa asilimia 79 ni salama hazina 
matatizo ya aina yeyote. 
Alidai
 kuwa kufuatia uzimaji wa simu bandia litakalofanyika juni 16 mamlaka 
hiyo imeweza kutoa elimu kwa wauzaji,watumiaji ili kuhakikisha kuwa 
wanabini simu zao kama ni salama ili kuweza kuepuka zoezi la kuzimiwa 
simu zao bila yawao kujiandaa. 
“Wakati
 tumeanza kubaini zoezi la kutambua simu feki tulibaini kuwa asilimia 30
 zilikuwa bandia ila kutokana na elimu iliyotolewa hadi February simu 
bandia zimepungua hadi kufikia asilimia 18 hii inaonyesha kuwa simu feki
 zilizoko sokoni ni chache mno “aliongeza .
Aidha
 Innocent alitaja faida za kuzimiwa simu bandia kuwa ni pamoja na 
kuongeza usalama mtandaoni kwa watumiaji wa simu ,kupunguza wizi wa 
simu  na kupunguza matukio ya uhalifu ambayo yamekuwa yakitumika mara 
nyingi kwa njia ya simu hizo pamoja na kuzuia matumizi ya simu zisizokuwa na viwango. 
Awali mkurugenzi mkuu wa mamlaka hiyo Ally Simba aliwataka wananchi kufanya
 zoezi la kuhakiki simu zao kwa kufuata maelekezo sahii ili waweze 
kubaini simu feki kabla ya kuzimiwa simu hizo juni 16 ,kwani wengi wa 
watumiaji wa simu hawafuati malekezo ya kutambua simu bandia . 
Simba
 aliseama kuwa ni vema wananchi wakatumia mfumo waliowekewa wa kubaini  
simu zao kama ziko salama kwani ifikapo juni simu zote bandia zitazimwa 
na kuwataka wafanyabiashara nao wawe makini pindi wanaponunua mizigo yao
 ya bashara ili kuepuka hasara watakazozipata wao na pia hasara 
watakazopata wanunuzi wa simu hizo 
No comments:
Post a Comment