Friday, April 22, 2016

WATENDAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA WATAKIWA KUTEMBELEA MAENEO YAO YA KAZI




 NAIBU waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mheshimiwa Selemani Jafo amewataka watendaji wa mamlaka za serikali za mitaa kuwa na utaratibu wa kutembelea maeneo yao ya kazi ili kujua changamoto zilizopo na kuzitatua.

Akizungumza na walimu wa shule ya msingi Nzuguni B mkoani Dodoma wakati wa ziara aliyoifanya Mheshimiwa Jafo amesema kuwa watumishi hawawezi kufanya kazi kwa ubora iwapo hawatakuwa wakitembelea na kukagua maeneo yao ya kazi.
Katika ziara yake amewataka walimu wa shule ya msingi Nzuguni B na Shule ya sekondari Nzuguni A kuweka utaratibu wa kujiwekea malengo na kujipima kuona walichokifanya ili kupata matokeo tarajiwa.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...