Friday, April 22, 2016

BARAKA DA PRINCE KUMSHIRIKISHA NAJMA KATIKA NGOMA YAKE MPYA


Staa wa muziki wa kizazi kipya Baraka Da Prince amesema ngoma yake mpya iitwacho ‘Twende’ ameimba kwa kumshirikisha mchumba wake Najma Dattan.
Staa huyo alisema kwamba kibao hicho tayari kimesharekodiwa na anatarajia kukisambaza kwenye vituo mbalimbalo vya redio nchini ili mashabiki wa muziki wa bongo flava waanze kuusikiliza.
”Sisi wote ni wasanii ndiyo maana tumeamua kushirikiana katika wimbo huu ambao una ujumbe maalum kwa Najma unaelezea safari ya kwenda kumtambulisha kwa wazazi wangu na tayari niemeshafanya hivyo,”alisema Baraka.
Msanii huyo aliongeza kwa kuwataka wale wanaozungumza taarifa za ‘Uzushi’ kuhusiana na maisha na mchumba wake waache kwa sababu kila anachokifanya na vitu anavyotumia ni mali yak na si via kuazima.
Baraka alisema kuwa wanaomsema vibaya ni wapinzani wake na hiyo haiwezi kumkatisha tamaa kwenye safari yao ya mafanikio waliyoianza

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...