Saturday, April 23, 2016

GITAA KUACHIA AUDIO NA VIDEO MPYA KWA PAMOJA, MKONO WA ABY DADY


Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Gitaa Supertalent ambaye alishawahi kusumbua na kibao chake matata sana kinachoitwa Homa ya Mapenzi hivi karibuni anatarajia kuachia ngoma mpya ambayo imesimamiwa na mikono salama ya mtayarishaji mkali wa muziki wa kizazi kipya hapa Bongo Aby Dady. Track hiyo mpya ipo katika hatua za mwisho ya kukamilika kwa video yake ambayo itakuwa na viwango vya kimataifa. 

Kwa mujibu wa Gitaa ambaye ni mkali wa masauti jina la track hiyo bado halijawekwa wazi ila ipo katika hatua ya mwisho kukamilika kwa hiyo wapenzi wa mziki mzuri wakae tayari kwa mkao wa kula kwa ajili ya kupokea mziki mzuri kutoka kwa kijana mwenye kipaji cha hali ya juu Gitaa Supertalent.



No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...