Basi la wachezaji wa soka TZ lakamatwa ili kulipa madeni
Basi la wachezaji wa timu ya 
taifa ya Tanzania, limekamatwa kwa amri ya mahakama kutokana na deni la 
shilingi milioni 140 (zaidi ya dola 85,000), ambalo kampuni ya Punchline
 kutoka Kenya, inadaiwa kulidai shirikisho la kabumbu Tanzania (TFF).
Madalali ndiyo walilikamata basi hilo likiwa kama dhamana huku TFF ikitakiwa kulipa deni husika kabla ya kurejeshewa mali zao.
Msemaji wa Shirikisho la Soka 
Tanzania (TFF), Boniface Wambura, amesema tayari wamelipa shilingi 
millioni 70 ikiwa ni malipo ya awali.
Deni hilo linatokana na gharama za uchapishaji 
tiketi za kuingilia uwanjani katika mechi za ligi kuu ya Tanzania tangu 
mwaka 1997.
TFF kwa sasa iko katika mpango wa kuuza tiketi 
za uwanjani kwa njia ya ki-eletroniki (umeme) ikiwa ni sehemu ya 
jitihada ya kupunguza adha kwa wapenzi wa soka na kudhibiti wizi na 
ulanguzi wa tiketi.
Wambura amesema jitihada zinafanyika kumaliza 
deni hilo, ila TFF italifuatilia kwa umakini na kuchunguza mwenendo 
mzima uliosababisha kuwepo deni hilo.

No comments:
Post a Comment